Matukio Yajayo
Mkutano wa Kiasasi wa Kitaifa Apr 10, 2026
Mkutano Mkuu wa Kitaifa Apr 24, 2026

Kuhusu Imani

About Us

Imani ya Kibaháʼí Tanzania

Imani ya Kibaha'i ni dini ya Ulimwengu inayofundisha umoja wa Mungu, umoja wa dini, na umoja wa binadamu wote. Ilianzishwa na Mdhihirishaji wa Mungu kwa wakati huu Bahá'u'lláh mwaka 1844, ambaye alitambulisha ujumbe wa kiroho unaolenga kuunganisha wanadamu na kujenga dunia yenye haki, amani, na ustawi wa pamoja. Wabaha'i wanaamini kuwa Mungu ametuma Waangalizi Wake katika nyakati mbalimbali—kama vile Ibrahimu, Musa, Krishna, Buddha, Yesu Kristo, Muhammad, na Bahá'u'lláh—ili kuwaongoza wanadamu katika safari yao ya kiroho na maendeleo ya ustaarabu. Imani ya Kibaha'i inasisitiza kanuni kama vile usawa wa wanawake na wanaume, elimu kwa wote, uondoaji wa ubaguzi wa rangi na dini, uadilifu wa kiuchumi, na uongozi wa haki unaotegemea mashauriano na huduma. Lengo lake kuu ni kujenga jamii inayodhihirisha upendo, umoja, na maendeleo endelevu ya kiroho na kimwili.

Imani ya Kibaha'i nchini Tanzania ilianza kupokelewa katika miaka ya 1950, na tangu wakati huo imeendelea kuenea kwa kasi katika mikoa mbalimbali ya nchi. Leo, Wabaha'i wa Tanzania wanashiriki katika juhudi za kijamii, kielimu, na kiroho zinazolenga kuboresha maisha ya watu wote bila ubaguzi. Shughuli kama madarasa ya watoto, programu za vijana chipukizi na vijana, na Mikutano ya Ibada na mashauriano ya jamii zinachochea moyo wa umoja na huduma. Kupitia kanuni za "Umoja katika Utofauti" na "Huduma kwa Ubinadamu," Wabaha'i nchini Tanzania wanaendelea kushirikiana na watu wa dini, tamaduni, na mataifa yote katika kujenga jamii yenye uadilifu, matumaini, na upendo—jamii inayodhihirisha maneno ya Bahá'u'lláh: "Dunia ni nchi moja, na wanadamu ni raia wake."

Maendeleo ya Kiroho

Kuchangia katika mabadiliko ya jamii kupitia elimu ya kiroho na mikutano ya ibada.

Kujihusisha na Mijadala

Mijadala kuhusu masuala mbalimbali ya kijamii, hasa elimu, mazingira, usawa wa kijinsia na umoja wa binadamu

Jitihada za Kijamii na Kiuchumi

Kupitia elimu, shughuli za kijamii, na mikutano ya ibada, tunaimarisha jamii kote Tanzania.

Maktaba

Pata na uangalie Maandiko Matakatifu, Vitabu, Barua, Miongozo, Nyimbo na nyenzo nyinginezo mtandaoni

Maneno ya Mungu
PDF Sala
Idhini ya wazazi kwa ajili ya ndoa ya Kibahá’i
PDF Makusanyo
Nyenzo za Makongamano ya Kiulimwengu - Tanzania
PDF Nyenzo za Kujiongezea Elimu
Mfuko wa Kibahá’í
PDF Nyenzo za Kujiongezea Elimu
Nyumba ya Haki ya Ulimwengu
PDF Makusanyo
Maisha ya Ubikira na Matakatifu
PDF Makusanyo
Utakatifu wa Chaguzi za Kibahá’í
PDF Nyenzo za Kujiongezea Elimu
4 Januari 2026: Kwa Wabahá’í wa Ulimwengu
PDF Jumbe za Nyumba ya Haki ya Ulimwengu

Blogu

Habari mpya, ujifunzaji, na tafakari za hivi karibuni kutoka kwa jumuiya yetu

MKUTANO WA USHAURIANO JUU YA FASIHI ZA KIBAHA'I Events
Oct 24, 2025 843

MKUTANO WA USHAURIANO JUU YA FASIHI ZA KIBAHA'I

Mkutano wa mashauriano wenye hamasa na msukumo kuhusu kazi za fasihi za Kibahá’í ulifanyika 25-29 Septemba 2025 Bah...

Soma Zaidi
Umoja wa Binadamu Teachings
Oct 01, 2025 866

Umoja wa Binadamu

Imani ya Baha'i inafundisha kwamba wanadamu ni familia moja na wakati umefika kwa muungano wake katika jamii moja ya kim...

Soma Zaidi

Wasiliana Nasi

Wasiliana nasi - tungependa kusikia kutoka kwako

Anwani

P.O.Box 585-Dar es Salaam

Simu

+255 685 637 422

Barua Pepe

secretariat@bahai.or.tz